Thursday, 27 June 2019

Msanii Jaguar Kuendelea Kusota Rumande

Mbunge wa Kenya aliyekamatwa kwa kutoa maneno ya chuki dhidi ya wafanyabiashara wa kigeni atabaki rumande kwa siku ya pili wakati dhamana yake ikishughulikiwa.
Polisi walimfikisha Charles Njagua Kanyi maarufu Jaguar mahakamani hii leo lakini hakusomewa mashtaka.Kwa mujibu wa Mahakama, uchunguzi unafanyika kuhusu madai ya kupanga kuvamia mali za watu na kuwashambulia raia wa kigeni walio nchini Kenya.
Muendesha mashtaka ameitaka mahakama kuendelea kumshikilia mshukiwa kwa majuma mawili wakati wakimalizia uchunguzi wao.
Mahakama itatoa uamuzi kuhusu ombi la dhamana ya Jaguar kesho.

No comments:

Post a Comment