Friday, 28 June 2019

#TEKNOLOJIA:Watumiaji Wa Whatsapp GB & PLUS Kufungiwa

Zoezi la WhatsApp kuwafungia kwa muda watumiaji wa GB WhatsApp na WhatsApp Plus lilianza takribani miezi miwili iliyopita limezidi kuchachamaa, na sasa kampuni ya WhatsApp imetoa angalizo kwa wale ambao hurudi tena kwenye apps hizo tena na tena.

Katika taarifa rasmi iliyotolewa na WhatsApp – inayomilikiwa na kampuni ya Facebook, wamesema “kama unapokea ujumbe ndani ya app ikisema akaunti yako imefungiwa kwa muda (temporarily banned) ina maanisha unatumia toleo lisilo rasmi la WhatsApp.

Tayari Facebook wameonesha wapo njiani kukaribisha matangazo kwenye app ya WhatsApp na hivyo uwepo wa matoleo ya WhatsApp ambayo si rasmi ni hatari katika mpango wao huo. Ila pia ni matoleo ambayo data za mtumiaji zipo kwenye hatari ya udukuzi.

No comments:

Post a Comment