Wednesday, 3 July 2019

#SPORTS:Timu Zilizofanya Vibaya AFCON 2019,Tanzania & Namibia Zaongoza

Jumla ya timu nane zimefungasha virago kwa kutolewa katika hatua ya makundi, tatu kati ya hizo zimefungwa mechi zote.
Tanzania ndiyo timu iliyofanya vibaya zaidi katika mashindano hayo kitakwimu.
Tanzania imefungwa jumla ya magoli nane na kufunga mawili, hivyo wamemaliza wakiwa na uwiano wa magoli wa -6.

Timu inayofuata kwa kufanya vibaya ni Namibia ambayo pia ilifungwa mechi zote na kumaliza na uwiano wa magoli wa -5, kisha Burundi yenye alama sifuri pia na uwiano wa magoli wa -4.
Timu nyengine zilizofungasha virago ni Guinea-Bissau yenye alama 1, Zimbabwe alama 1, Mauritania alama 2, Angola alama 2 na Kenya yenye alama 3.
Timu nne zimefuzu katika raundi ya mtoano kama timu bora kati ya wale walioshindwa. Mataifa hayo ni Guinea, DR Congo, Afrika Kusini na Benin.

No comments:

Post a Comment